Friday 22 February 2013

ONYO KWA WAKAAZI WA GARISSA KUTOKA KWA MZALENDO KIBUNJA

Mwenyekiti wa tume ya uwiano na maridhiano NCIC Bw. Mzalendo kibunjia amewaonya wakaazi wa Garissa dhidi ya Ubaguzi wa kikabila,akizungumza katika mkutano  na wakaazi wa kaunti ya Garissa hapo jana.Mzalendo kibunjia alisisitiza kwamba ubaguzi wa wakenya haswa wale ambao si wa asili ya kisomali ni jambo ambalo halifai na linafaa kukemewa kabisa.Katika hotuba yake kibunjia aliwaomba wanainchi wa Garissa kupuuza matamshi ya baadhi ya watu na viongozi yanayosambaratisha uhusiano mzuri uliopo kati ya wakenya walio na asili ya kisomali na wale wasiokuwa wasomali huku akisema kuwa wakenya wanafaa kuwa mstari wa mbele kuheshimu na haki na maslahi ya kila mtu.

No comments:

Post a Comment