Sunday 19 July 2015

MSIKILIZE DAZLAH AKIZUNGUMZIA MZIKI WAKE PAMOJA NA COLLABO YAKE NA MSANII MKUBWA WA NAIROBI

Msanii kutoka studio ya TEE HITS kwa jina la DAZLAH KIDUCHE huenda ikawa sio kichwa kigeni katika skio lako kama wewe ni mfuatiliaji makini wa mziki wa pwani.Msanii huyu mwenye umri mdogo saana amechipuka na kukua kwa kasi ya juu saana katika tasnia ya mziki wa pwani na kufikia sasa, licha ya kuwa ni msanii aliyeanza mziki miaka ya juzijuzi,kwa wakati huu amewapiku baadhi ya magwiji na kuandikisha jina lake katika orodha ya wasanii wachache wanaowakilisha mziki wa pwani kitaifa na kufikia sasa tunaweza kusema kimataifa
Katika siku za hivi majuzi msanii Dazlah ameonekana kuwa mmoja ya wale wasanii wanaojituma saana na kuwekeza kwenye mziki kuanzia upande wa studio,mauzo pamoja na kazi zenye akili ili kukidhi mahitaji ya soko gumu la muziki.

Huyu apa dazlah msikilize akizungumzia mengi kuhusu mziki wake, siri ya mafanikio yake pamoja na collabo yake na msanii mmoja maarufu wa Nairobi.
 bonyeza hapa kumskiliza LISTEN

No comments:

Post a Comment