Wednesday 19 June 2013

BUDGET YA TANARIVER KAUNTI…18 June 2013



Kaunti ya Tana River imetenga shilling million ishirini (20,000,000) kwa sekta ya elimu, shilling million saba (7,000,000) kwa sekta ya mifugo na shilling million mia mbili (200,000,000) kwa sekta ya usafi na maji. Haya yamejiri katika kikao cha kukadiria bajeti ya County ya Tana River kilicho andaliwa hapo jana katika ukumbi wa Madogo Social Hall.
Akiongea  wakati  wa kikao hicho naibu wa mwenyekiti wa kamati ya budget bwana HUSSEIN GOBU GODHANA, alisema kuwa afisi ya Gavana wa Tana River ingependa kuhusisha wananchi wote wa Kaunti hii katika bajeti hiyo.Na kwa upande wake mwakilishi wa ward ya Madogo, ABDI ERIGAMSO alikosoa bajeti iliyopendekezwa kwa kusema haikumhusisha mwananchi wa kawaida. Aidha Abdi Ergamso amesema bajeti hiyo haijatenga kando fedha za mikasa, kama vile mafuriko na baa la njaa. Akiongezea, Abdi Ergamso aliomba fedha zitengwe kwa ajili ya elimu ya chekechea akisisitiza elimu ya chekechea ndio msingi wa elimu.

No comments:

Post a Comment