Wednesday 19 June 2013

MGOMO WA WALIMU…

 
Masomo katika shule zote za upili za  uma katika kaunti ya Tana River na Garissa  yanaendelea hata baada ya mgomo kuitishwa  na chama cha walimu wa shule za upili cha KUPPET.
Hii imebainika baada ya uchunguzi Tuliofanya hapo jana. Katika baadhi ya shule tulizo tembelea  tulikuta masoma yakiendelea  kama  kawaida.Katika shule ya upili ya Garissa High naibu mwalimu mkuu  Bw. Abdikarim Mohamed alitueleza kuwa wana subiri usemi  na ufafanuzi  zaidi kutoka kwa chama chao cha KUPPET.Ingawaje shule tulizotembelea katika kaunti ya Garissa na Tana River zilikuwa zikiendelea na masomo kama kawaida,  muungano  wa KUPPET unasisitiza kuwa mgomo uko na utaendelea.Haya yakijiri viongozi wa muungano wa walimu: KNUT, walisema hawatafanya mazungumzo na serikali kuhusu pesa za marupurupu wanazo idai serikali.



No comments:

Post a Comment