Thursday 30 October 2014

MAANDAMANO BURKINAFASO



Rais wa taifa la Burkina faso Blaise Compaore ametangaza hali ya dharura na kuvunjilia mbali serikali ya taifa hilo baada ya maelfu ya wanainchi kuandamana na kuchoma majengo ya bunge.Maandamano hayo yaliyotokea alhamisi ya tarehe 30 Novemba yamesababishwa na  mabadiliko ya katiba yaliyopendekezwa ili kumruhusu rais wa taifa hilo  kubakia mamlakani kwa muhula mwingine.waandamanaji hao walivamia kituo cha televisheni cha taifa pamoja na majengo mengine ya serikali.Ni maandamano yaliyosababisha takriban watu wawili kupoteza maisha huku rais akitangaza hali ya dharura na  kuitisha mazungumzo na viongozi wa upinzani ili kutafuta suluhisho ya hali ilivyo.Kufikia sasa hali ya taharuki inazidi kushuhudiwa katika taifa hilo.

No comments:

Post a Comment