Thursday 11 October 2012

HOFU YA MACHIFU GARISSA KUHUSU MFUMO WA KAUNTI

Machifu wa kaunti ya Garissa leo walikongamana katika afisi za wilaya ya Garissa kulalamikia hatima yao wakati serikali za kaunti zitakapoanza kufanya kazi.Aidha machifu hao walielezea hofu yao ya kuwa serikali huenda ikatupilia mbali kazi zao punde tu serikali za kaunti zitakapoanza kazi.Hata hivyo machifu hao wanataka wadhifa wao ubainishwe wazi kikatiba kama vile wadhifa wa kamishna wa kaunti unavyotambuliwa na wanainchi kote inchini

No comments:

Post a Comment