Thursday 18 October 2012

UKULIMA KATIKA KINGO ZA MTO TANA

Leo tukajipata MCHELELO FARM moja ya mashamba yaliyoko kando ya mto tana.Tumetambua huko maskani maswala na ukulima yamepewa kipau mbele saana.Washkaji kibao wanautumia vizuri mto tana ndio maana licha ya jua kali linalowaka tana river na Garissa kiujumla bado kuna uwezekano wa kupata mimea mingi saana ikifanya vizuri katika maeneo haya yaliyo kando na mto na hata yale yaliyombali iwapo tutakumbatia ukulima wa unyunyiziaji maji kutoka mto huo.Kulingana na hali ilivyo katika kingo za mto tana ni kwamba vipo vipande vingi saana vya ardhi ambavyo endapo vitatumiwa vizuri basi tatizo la uhaba wa chakula katika maeneo ya Tana river na Garissa litapungua kwa kiwango kikubwa saana.Ndani ya mchelelo farm kuna mimea mingi saana kama vile sukuma,mchicha,mabiringanya,mabamia/mabenda,Tomato,mahindi,ndizi,vitunguu,miwa na mimea mingi saana ikiwa ni dhihirisho kubwa kuwa ardhi hii iko na rutuba ya kutosha kuweza kuhimili ukuaji wa mimea mingi tofauti.Hata hivyo kila kizuri huwa hakikosi changamoto kwani mbali na kuwepo kwa unawiri mzuri wa mimea tatizo ni kwamba zao lao mara nyingi huharibika shambani kwa sababu wa uosefu wa wanunuaji kwani eneo hilo ni mbali saana na sokoni hivyo basi zao linapokua tayari mara nyingi huozea shambani kwani kulifikisha sokoni huwa ni ngumu saana...HIZI HAPA BAADHI YA PICHA ZA ENEO HILO

TANA RIVER


                                                                NDIZI
                                                                          MIWA
                                                                PUMPKINS
                                                                      VITUNGUU
                                                              MAHINDI
                                                     MABIRINGANYA
                                                       TOMATO
                                                                  SUKUMA
                               NIKAAMUA PIA KUPOZ NA WAKULIMA WENYE 
                                               KUSABABISHA  USTAWISHAJI HUU

No comments:

Post a Comment