Friday 12 October 2012

WATOTO WAWILI WAZAMA KATIKA MTO TANA KARIBU NA MORORO

Shughuli za uokoaji bado zinaendelea katika mto tana karibu na mororo baada ya watoto wawili kuzama walipokuwa wakiogelea hapo jana mwendo wa saa kumi.Aidha kwa sasa mwili wa mtoto mmoja mvulana mwenye umri wa takriban miaka tisa umepatikana hii leo majira ya asubuhi.Kulingana na taarifa,watoto hao wawili walizama katika mto huo walipokua wakiogelea.Hata hivyo shughuli za kumtafuta mtoto mwingine ambaye bado hajapatikana bado zinaendelea

No comments:

Post a Comment