Saturday 6 October 2012

OCPD WA GARISSA NA MAAFISA KUMI WA POLISI WAFUTWA KAZI

OCPD wa Garissa Felix munyambu na maafisa wengine wa usalama kumi wamefutwa kazi kwa tuhuma za kuruhusu washukiwa wawili wa kigaidi kuingia humu inchini na silaha hatari mnamo may tarehe nne mwaka huu.Mbali na munyambu,kuna maafisa wengine kumi waliofutwa kazi,sita wakitoka katika kitengo cha regular police huku wanne wakitoka katika kitengo cha AP waliokua wakishika doria katika kivukio cha Tana(tana bridge).Baadhi ya washukiwa wa ugaidi waliopita katika kivukio hicho cha tana walinaswa matuu wakiwa na kilo nane za vilipuzi,
waziri wa usalama Ole metito amewasihi maafisa wa polisi wawe wazalendo katika kazi yao ili waweze kuimarisha usalama wa wakenya.Metito pia alimuamuru kamishna wa polisi awapandishe ngazi maafisa walionasa vilipuzi huko matuu.

No comments:

Post a Comment